UMOJA WA WATANZANIA UJERUMANI KUSHIRIKI MAONYESHO YA KIMATAIFA MJINI ASCHAFFENBURG.




Umoja wa Watanzania Ujerumani (U.T.U ) Kushiriki katika Festival ya
"Brüderschaft der völker " mjini      Aschaffenburg " Ujerumani.
                   Kuanzia 19 hadi 21 Julai 2013

Watayarishaji wa Festival ya "Brüderschaft der völker " mjini Aschaffenburg,
nchini Ujeruamani,wameuhalika Umoja wa Watanzania Ujerumani (UTU) kushiriki katika maonyesho hayo utamaduni wa nchi mbali mbali yatakayo
anza 19 hadi 21 Julai 2013.

Watayarishaji wa maonyesho hayo wamevutiwa sana sana na shughuli
za Umoja wa Watanzania ujerumani (UTU) kwa juhudi zake za kuitangaza
Tanzania,wandaaji wa onyesho hilo wametoa nafasi kwa umoja wa watanzania kushiriki na kuitangaza Tanzania kwa kasi zaidi.
Mwenyekiti wa UTU Bw.Mfundo Peter Mfundo ameupokea mwaliko
huo kwa mikono miwili na amewaomba Watanzania wote wanaoishi
ujerumani kujitokeza kwa wingi katika maonyesho hayo na kuitumia
nafasi waliyopewa kwa maslahi ya Tanzania na watanzania, Umoja wa
Watanzania (UTU) utakuwa na banda lake katika maonyesho hayo.
Mnakaribishwa wote na kwa maelezo zaidi wasiliana na


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment